TARI YAGUNDUA MBEGU MPYA 16 ZA KOROSHO NA KARANGA
.....................
Na Mwandishi Wetu
DAR ES SALAAM; Taasisi ya Utafiti wa Kilimo Tanzania (TARI), imegundua
mbegu mpya 16 za mazao ya maharage, korosho na karanga zitakazoanza kutumika
msimu wa kilimo mwaka 2024/2025.
Mbegu hizo mpya ambazo zimeidhinishwa na Kamati ya Taifa ya Mbegu zimefanyiwa
utafiti na kugundulika kuwa zinasifa za kutoa mavuno mengi, kuwa na ukinzani
dhidi ya magonjwa na kukomaa mapema.
Mbegu hizo ni pamoja na aina sita za maharage; TARIBEAN6, TARIBEAN 7,
TARIBEAN 8, TARIBEAN 9, TARIBEAN 10, TARIBEAN 11 na karanga aina mbili ambazo
ni TARIKA 1 na TARIKA 2.
Pia katika zao la korosho jumla ya aina nane za mbegu bora za Korosho zimegunduliwa ambazo ni TARIKO-1, TARIKO-2, TARIKO-3, TARIKO-4, TARIKO-5, TARIKO-6, TARIKO-7 na TARIKO- 8.




No comments