Header Ads

WETCU TABORA YAWEKA MAKISIO YA UZALISHAJI KILO ZAIDI YA MILIONI 67 MSIMU WA KILIMO WA 2024/ 2025


 Muonekano wa shamba la Tumbaku.

 ..........................

Na Hastin Liumba,Tabora

CHAMA  Kikuu cha Ushirika cha wakulima wa zao la Tumbaku Kanda ya Magharibi (WETCU 2018 LTD) mkoani Tabora kimeweka makisio ya uzalishaji wa zao la tumbaku kwa msimu wa mwaka 2024/2025 ni kilo milioni zaidi ya milioni 67.

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake meneja Samweli  Jokeya alifafanuakuwa msimu ujao makisio ya uzalishaji yatakuwa ni kilo zaidi 67 kulingana na hali ya kijiografia itakavyokuwa.

Akiongea zaidi kuwa WETCU inabeba vyama vya Amcos mkoa wa Tabora,Ujyui, na Nzega ambapo awali katika msimu uliopita kilimo makiso yalikuwa ni kilo milioni 47 lakini uzalishaji ukaja kufikia kilomilioni 25 na hali hiyo ilitokana na hali ya kijigrorafia Ilivyokuwa.

Aidha aliongeza kusisitiza kuwa kutokana na mvua nyingi zilivyokuwa na kunyesha tumbaku nyingi ziliharibika na kukosa ubora na kupelekea zao hilo kukosa ubora wa kimadaraja kama kanuni za kilimo cha za o la tumbaku zinavyoelekeza.

Jokeya alisema eneo kubwa la uzalishaji wa zao la tumbaku kuwa liligubikwa na matatizo mengi ambayo makisio tuliyopanga kwa msimu ujao hivyo malengo yetu hayakutimia.

Katika hatua nyingine meneja Jokeya alisema katika msimu wa mwaka 2024/2025makisio yatakuwa kilo milioni 67 lakini tumejipanga kuhakikisha makisio hayo yanaongezeka na nsiyo kupungua ili vyama vyetu vilivyo chini ya WETCU vinufaike zaidi.

Meneja huyo alifafanua zaidi kuwa katika msimu yliopita wa mwaka 2023/2024 kulikuwa na mbolea na pembejeo ambazo baadhi siyo zte kukosa ubora hali ambayo ilileta hasaea kwa wakulima wetu na kukosekana kwa malengo waliyokusudiwa kimsimu.

Aidha alisema na kuomba mamlaka husika kuhusiana na usambazaji  wa mbolea na pembejeo zifike kwa wkati ili mkulima wa zai hilo afanye kazi zake za kilimo wa wakati.

Jokeya alisema kwa sasa kama chama kikuu wamekuwa wakiaagiza kamba za ufungaji tumbaku toka nchi za India na Banladesshi na hapo ndipo kunakuwa na gharama nyingine kiuzalishaji tunayopata kiutendaji kama WETCU kwa vyama vyetu vya Amcos.

Hata hivyo alisema kuwa wapo wakulima ambao kimsingia ni changamoto ambayo wanatorosha tumba na hiyo ni wizi,wadanyanyifu na waovu.

Aidha aliongeza wakulima hao wengine wamekamatwa na kupelekwa kwenye vyombo vya sharia kwa uchunguzi unaendelea.

Alisisitiza kuwa msimu uliopita kulikuwa na changamoto kadhaa nyingine ikiwemo baaadhi ya wakulima kutorosha tuma,mvua nyngi kiasi mkwamba tumbaku kukosa thamani halisi inayotakiwa maana mengine kulikuwa na mvua za mawe.

Jokeya alisema changamoto nyingine kama nilivyosema ni ubora wa mbolea lakini naiomba serikali kupitia mamlaka husika pembejeo na mbolea kufikawaka tin a hii itasaidia kuongeza thamani ya zao la tumbaku kimadaraja.

Alisema na kuwashauri kupitia vyama husika kuaandaa mashamba yao mapema tayari kwa msimu ujao wa kilimo na kuwashauri pia wasahao kilimo cha mazao mbadala hasa ya chakula kwa ajili ya kilimo.

No comments

Powered by Blogger.