Header Ads

COMRADE REHEMA SOMBI AKOSHWA NA MRADI WA UFUGAJI SAMAKI KWA NJIA YA VIZIMBA

 Makamu Mwenyekiti wa UVCCM Taifa, Rehema Sombi, akielekea kukagua mradi wa ufugaji wa samaki kwa kutumia vizimba.

....................................

Na Mwandishi Wetu

Makamu Mwenyekiti wa UVCCM Taifa, Rehema Sombi ameonesha kufurahishwa na vijana Wanufaika wa Mradi wa ufugaji wa samaki kwa njia ya vizimba waliopo Mtaa wa Kisoko, Luchelele Wilaya ya Nyamagana Mkoani Mwanza baada kuwatembelea na kuona maendeleo mazuri yaliyofikiwa na vijana hao tangu walivyokabidhiwa vizimba hivyo na Mhe. Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan, mwezi Januari 30, 2024.

Comrade REHEMA aliwaeleza vijana hao kuwa maono ya Mhe. Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan ni kujenga kesho iliyobora kwa vijana hivyo Mradi huo wa vizimba ni sehemu ya hatua anazoendelea kuzichukua katika kuhakikisha vijana wanajikomboa kimaisha kupitia fursa zilizopo kwenye sekta ya uvuvi.

Aliongeza kwa kuwataka vijana hao kuongeza bidii katika ufugaji wao kwani watapokuwa wamefanya vyema itakuwa ndio mwanzo wa kuvutia uwekezaji zaidi katika tasnia hiyo ya ufugaji samaki kwenye vizimba.

Akitoa maelezo kwa niaba ya vijana hao, Katibu wa Wanufaika wa Vizimba Wilaya ya Nyamagana Ndg Omary Mangu alisema, eneo Hilo la Kisoko pekee Lina Vikundi 18, wenye Vizimba 112 na vifaranga vya samaki Million 1.5 na tayari wameanza kuvuna samaki tokea Septemba 23, 2024 jambo ambalo limewawezesha kurudisha nusu ya mkopo kupitia Benki ya Maendeleo ya Kilimo (TADB).

Katika ziara hiyo, Comrade Rehema aliongozana na Mwenyekiti wa UVCCM Mkoa wa Mwanza Ndg. Seth Masalu na Mbunge wa Vijana Taifa Mhe Ng'wasi Kamani.

Hapa akipata maelezo ya mradi huo.
Safari ya kutumia boti maalumu ikifanyika wakati wa kutembelea mradi huo.

No comments

Powered by Blogger.