UNGA LISHE WA KAMPUNI YA LONG LIFE GROUP CO. LTD WAVUTA WENGI SABASABA
Wadau na Wanafunzi wa ST, Rosalia School Nursery Primary and Secondary ya Kinyerezi Tabata Zimbili wakiwa kwenye Banda la Kampuni ya Longlife Group Co.Ltd wakinunua unga lishe na uji lishe uliopikwa katika Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara Dar es Salaam Sabasaba Julai 10, 2026.
............................................
UNGA wa
lishe unaotengenezwa na Kampuni ya Long Life Group Co. Ltd kutokana na ubora
wake umekuwa kivutio katika Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara Dar es
Salaam Sabasaba.
Unga huo
ambao unaitwa Afya Meal ni mzuri kwa afya unatumiwa na watoto kuanzia miezi
sita na watu wazima una mchanganyiko wa mahindi lishe, mbegu za maboga, mbegu
za mchicha, maziwa soya na mbegu za chia.
Kampuni hiyo
ndiyo mzalishaji na msambazaji mkuu wa bidhaa za chakula nchini Tanzania.
Kampuni hiyo
inajulikana kwa kutengeneza unga wa lishe wenye chapa ya LF Lishe (Long Life
Natural Foods), unaolenga kujenga afya ya familia na jamii.
Aina za Unga
wa Lishe kutoka Long Life Group LF Nutritious Porridge (Unga wa Uji wa Lishe).
Unga huo ni maalumu
uliotengenezwa kwa ajili ya kupika uji uliosheheni virutubisho na umelainishwa
vizuri ili uwe rahisi kuyeyuka tumboni, ukitoa nguvu na kusaidia ukuaji bora wa
watoto pamoja na watu wazima.
Unga
mwingine unaotengenezwa na kampuni hiyo ni LF Dona Lishe (Unga wa Ugali wa
Lishe)
Huo ni unga
wa ugali ulio na virutubisho vya asili
(bio-fortified) kwa ajili ya kulinda na kuimarisha afya za familia kupitia mlo
mkuu wa ugali.
Katika
Maonesho ya Sabasaba yanayoendelea jijini Dar es Salaam mamia ya watu wazima na watoto wamekuwa wakifurika katika banda la kampuni hiyo kwa ajili ya kununua
unga huo uliowekwa kwa viwango mbalimbali na unauzwa kwa bei nafuu ambao upo kuanzia kilo moja, nusu kilo na robo
Mbali ya
kuuzwa pia wateja wamekuwa wakinunua uji uliopigwa ambao unauzwa katika banda
hilo.Wanafunzi wakiwaa katika banda laa kampuni hiyo wakisubiri kupewa uji lishe.
Wanafunzi wa shule hiyo wakinywa uji lishe uliotengenezwa na kampuni hiyo
Mmoja wa wahudumu wa kampuni hiyo aliyefahamika kwa jina moja la Emmy akiwajibika katika maonesho hayo.
Taarifa hii imeandaliwa na Dotto Mwaibale simu namba 0754362990.


No comments