KILIMO BORA CHA MAEMBE
·
Maembe hulimwa kwa wingi katika mikoa ya Tabora, Pwani, Mtwara, Tanga, Mwanza, Morogoro na Mbeya. Uzalishaji wake ni wastani wa tani 159,472 kwa mwaka. Maembe ni zao muhimu la biashara na chakula.
MAMBO YA KUZINGATIA WAKATI WA UZALISHAJI
Ili kupata mazao bora ni muhimu kuzingatia kanuni bora za kilimo cha maembe hasa kanuni
zifuatazo:
Kuchagua aina bora ya kupanda kulingana na mahitaji ya soko.
Panda umbali wa mita 10 kwa kumi kama utatumia miembe ya kuunga, hii ni kwa sababu haiwi mikubwa sana kwa sababu haiishi miaka mingi, kwa ile ambayo si ya kuunga panda umbali wa mita 15 kwa 15 kwa kila mti mmoja wa muembe
DHIBITI MAGONJWA, WADUDU, NA MAGUGU
• Fanya ukaguzi wa shamba mara kwa mara ili uweze kudhibiti wadudu na magonjwa ya matunda kabla madhara hayajawa makubwa
UGONJWA WA KUTU KWENYE MAJANI
• Ni muhimu kudhibiti wadudu, magonjwa na magugu ili kupata mazao bora ambayo yatapata soko zuri na kuweza kuhifadhiwa kwa muda mrefu.
• Hakikisha shamba ni safi wakati wote ili kupata matunda bora na kurahisisha uvunaji.
MAANDALIZI KABLA YA KUVUNA
Kusafisha shamba pamoja na barabara za shamba
• Safisha shamba ili kurahisisha uvunaji na usafirishaji shambani.
Kukagua shamba kuona maembe kama yamekomaa Maembe hukomaa katika kipindi cha miezi 4 hadi-6 tangu kutoa maua kutegemea hali ya hewa na aina.
DALILI ZA MAEMBE YALIYOKOMAA
• Maembe hung’ara
• Kwa aina nyingine rangi ya kijani hufifia na kuanza kubadilika kuwa ya manjano.
ANDAA VIFAA VYA KUBEBEA, SEHEMU YA KUFUNGASHIA NA USAFIRI.
VIFAA VYA KUBEBEA
• Ngazi
• Vikapu
• Mifuko
• Ndoo
• Vichumio
VIFAA VYA KUFUNGASHIA
• Makasha ya mbao/plastiki na ya makaratasi magumu na matenga
VYOMBO VYA KUSAFIRISHIA
• Matoroli
• Magari
• Baiskeli
• Matela ya matrekta
KUVUNA
Njia bora ya kuvuna maembe ni Kuchuma kwa mkono
• Kwa miembe mifupi chuma maembe pamoja na kikonyo chake
• Kwa miembe mirefu chuma kwa kutumia kichumio maalumu
KICHUMIO MAALUM
• Acha kikonyo chenye urefu wa sentimita tatu hadi


No comments