Header Ads

ZIARA ZA WAZIRI BASHE MIKOANI ZALETA MATUMAINI KWA WAKULIMA

Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe, akiwa kwenye ukaguzi wa miradi mkoani Ruvuma. 

----------------------------------------

Imeandaliwa na Dotto Mwaibale / ( 0754-362990 )

KAULI ya Kilimo ni Uti wa Mgongo au kilimo ni uhai  haipingiki kwani maisha ya binadamu yanategemea chakula kinachotokana na shughuli za kilimo zinazosimamiwa na Wizara ya Kilimo.

Kuwepo kwa Wizara ya Kilimo pekee haitoshi bali ni viongozi gani waliopo katika wizara hiyo ambao wanawiwa na kuona  kilimo kinakuwa cha tija na kumnufaisha mkulima na Taifa kwa ujumla.

Leo Tanzania tuna Waziri wa Kilimo ambaye ni Mbunge wa Jimbo la Nzega kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Hussein Bashe. Kabla ya Bashe kuwa waziri,  katika wizara hiyo wamepita mawaziri wengi ambao kwa namna moja au nyingine kwa wakati wao walifanya vizuri na kuisogeza mbele sekta ya kilimo hapa nchini..

Rais wa Awamu ya Tano Hayati Dkt. John Pombe Magufuli ndiye aliyemuibua Bashe na kumpa nafasi ya kuwa Naibu Waziri wa Kilimo na hapo ndipo uwezo wa Bashe kwenye masuala ya kilimo ulipoonekana.

Katika kipindi kifupi alichohuduma kama Naibu Waziri wa Kilimo akiwa na Hayati Rais Maghufuli mafanikio kadhaa katika sekta ya kilimo yalianza kuonekana na kufurahiwa na wakulima baada ya kushusha bei za pembejeo na kupandisha bei ya mazao.

Baada ya Rais Samia Suluhu Hassan kuingia madaraka naye kwa kuzingatia kuwa kilimo ni uhai na kuuona uwezo wa Bashe kwenye masuala ya kilimo alimteua kuwa waziri kamili wa wizara hiyo.

Kuteuliwa kwa Bashe kuwa waziri kumemuongezea ari, nguvu na kuwa na mikakati mbalimbali ya kuhakikisha kilimo hapa nchini kinakuwa namba moja katika  kukuza uchumi wa nchi na wakulima kwa ujumla.

Waziri Bashe tangu amekuwa katika nafasi hiyo amekuwa akikutana na makundi mbalimbali ya wataalamu wa kilimo wa ndani na nje kwa ajili ya kupeana uzoefu kuhusu masuala ya kilimo na anayafanya hayo yote kutokana na kuwiwa na kazi hiyo.

Moja ya mkakati wake mkubwa ni kuona Tanzania inafanya kilimo cha umwagiliaji ambapo Serikali inayoongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan imekuwa ikitenga kiasi kikubwa cha fedha kuhakikisha jambo hilo linasonga mbele na ndio maana sasa tunaona kuna skimu nyingi za kilimo hicho sehemu mbalimbali.

Mkakati wake mwingine ni pale alipojenga hoja za kuishawishi Wizara ya Fedha na Benki kuu kuunda sera za kifedha ambazo zitakuwa rafiki kwa sekta ya kilimo.

Jambo lingine alilolifanya akiwa Naibu Waziri wa Kilimo ni kutekeleza agizo la Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kuhusu utambuzi wa wakulima ambapo hadi sasa kupitia Mfumo wa M-Kilimo tayari wakulima 1,979,662 na Maafisa Ugani 6,840 walisajiliwa kwenye mfumo hatua inayosaidia kufikisha huduma za ugani na masoko kwa haraka.

Katika hatua nyingine ya mikakati yake ya kuinua kilimo,Waziri Bashe aliwataka wadau wa zao la Tumbaku nchini kuwahamasisha wakulima wa zao hilo kulima mazao mengine kwenye maeneo yao badala ya kutegemea Tumbaku peke yake kauli aliyoitoa Februali 3, 2023 jijini Dodoma kwenye semina ya sheria na sera mbalimbali za Sekta ya Tumbaku iliyoshirikisha kampuni za ununuzi wa zao hilo, wakulima na wadau wengine.

Mbali ya kuwa na mikakati hiyo tabia yake ya kutoka ofisini na kwenda kuonana na wakulima kusikiliza kero na mahitaji yao imekuwa ikimsaidia kuongeza ufanisi wa kilimo kuanzia kwenye zana za kilimo, pembejeo na mahitaji yote yanayohusu kilimo.

Kushiriki kwa Maonesho ya kilimo, kuwawezesha maafisa ugani kwa kuwapa semina na vifaa vya kazi kama pikipiki ili kuwafikia wakulima ni eneo lingine ambalo linaongeza tija katika kilimo ambapo kwenye kipindi hiki cha Waziri Bashe tumeona kumekuwa na fursa nyingi zikitolewa kwa maafisa hao kwa ajili ya kuwasidia kuwapa mbinu bora za kilimo wakulima.

Binafsi naweza kusema kuwa Bashe  ni zawadi ya pekee tuliopewa Watanzania na Mungu kwa ajili ya kuliinua taifa letu kutokana na maono na utendaji kazi wake uliotukuka kwenye sekta hiyo ambayo tunaiona kwenye mataifa mengine duniani yakipiga   hatua kubwa ya kiuchumi.

Kutokana na kuwiwa huko na kutaka kuona Taifa la Tanzania kilimo kinakuwa ni chanzo kikubwa cha uchumi Waziri wa Kilimo Hussein Bashe yupo katika ziara mikoani ya kuzungumza na wakulima na kukagua miradi mbalimbali ya kilimo akiwa ameongozana na viongozi wenzake wa Taasisi mbalimbali zilizo chini ya wizara hiyo ambapo ametangaza fursa mbalimbali na kuwataka wakulima kuzichangamikia.

Ziara hiyo anayoifanya imeonesha kuwa na mafanikio na tija huku ikitoa matumaini makubwa kwa wakulima ambao walikuwa wamekata tamaa baada ya kuziona fursa kupitia kilimo.

Katika ziara hiyo Waziri Bashe amekuwa akizungumza na wakulima na kusikiliza maoni yao ambapo pia amekuwa akitoa  maelekezo ya papo kwa papo kwa ajili ya kuboresha kilimo.

Wananchi na wakulima wanaojitokeza kwenye ziara za Waziri Bashe wamekua wakionesha furaha zao za wazi huku wengine wakisema hawajawahi kumuona Waziri ambaye anatembea  kwa miguu muda mrefu kwenda walipo wakulima kuzungumza nao ili kujua changamoto zao kama anavyofanya.

Mpaka sasa Waziri Bashe na timu yake amekwisha fanya ziara katika mikoa ya Singida,Tabora, Simiyu na Ruvuma.

Binafsi Bashe na timu yako napenda kukutia moyo kwa kazi kubwa unayoifanya kwani Watanzania wapenda maendeleo wanaiona pia kumbuka kuwa hakuna kazi isiyo na changamoto songa mbele ukiendelea kumuheshimisha Rais Samia Suluhu Hassan aliyekuamini na kukupa nafasi hiyo ili siku moja vizazi vijavyo vije kuona alama ambayo utakuwa umeiacha kwenye sekta ya kilimo hapa nchini.

 Mungu akupe afya njema ili uendelee  kuwatumikia watanzania na Taifa kwa ujumla. Kazi Iendelee.

Waziri Bashe akiwa na watoto wakati wa ziara hiyo.
Waziri wa Kilimo Hussein Bashe akishiriki kupiga ngoma wakati wa ziara hiyo
Mbunge wa Jimbo la Nyasa, Mhandisi Stella Manyanya akizungumza wakati wa ziara hiyo.
Ziara ikiendelea.
Waziri Bashe akihutubia.
Waziri Bashe akitafakari jambo kwenye ziara hiyo.

No comments

Powered by Blogger.