Header Ads

MNYETI AMALIZA MGOGORO WA MUDA MREFU BAINA YA WANANCHI NA SHAMBA LA MIFUGO MABUKI

Mbunge wa Misungwi ambaye pia ni  Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi  Alexander  Mnyeti.

.................................................... .

Na Kingi Bashite, Misungwi Mwanza

MBUNGE wa Jimbo la Misungwi ambaye pia ni  Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi  Alexander  Mnyeti  amefanikiwa kumaliza mgogoro wa ardhi uliodumu kwa muda mrefu baina ya wananchi na shamba la mifugo Mabuki lililopo Wilaya ya Misungwi mkoani Mwanza.

Kwa muda mrefu matukio mengi yalikuwa yakiibuka mara kwa mara na kutishia usalama wa maisha ya watu kutokana na mgogoro huo.

Wananchi kutoka maeneo mbali mbali walikuwa wakiingiza mifugo yao katika shamba hilo  huku wakiwa na silaha za jadi kwa lengo la kutafuta malisho kwenye shamba hilo la serikali.

Kibaya zaidi hata watumishi wa Serikali wa shamba hilo walikuwa wanavamiwa na kupingwa na huku baadhi yao wakinusurika kuuawa nyakati za usiku.

Aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Mwanza ambaye sasa  ni Katibu wa Itikadi na Uenezi  wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Taifa,  Amos Makalla alifikia maamuzi ya kupeleka Kikosi cha Kuzuia Ghasia ( FFU ) lakini bado mgogoro huo haukumalizika.

Kutokana na mgogoro huo kuwa wa muda mrefu Mbunge wa jimbo la Misungwi ambaye pia ni Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi  Alexander Mnyeti  ameumaliza mgogoro huo baada ya kuja na njia nzuri.

Mnyeti akiwa katika ziara yake ya kikazi katika shamba hilo alitangaza kuumaliza mgogoro huo ndani ya mwezi mmoja ambapo baada ya kipindi hicho alichokiomba Serikali imezungushia uzio eneo lote la shamba hilo.

Hatua hiyo ya kuweka uzio kwenye shamba hilo umekuwa ni muarobaini wa kumaliza changamoto hiyo iliyokuwepo kwa muda mrefu kwani hivi sasa hakuna tena muingiliano wa watu kugombea eneo hilo.

Katika shamba hilo zinafanyika shunguli tatu tofauti ambazo ni

1:Shamba la Mifugo Mabuki ( Chuo cha Mifugo Mabuki )

2: Programu ya Jenga Kesho iliyo bora  yaani Building Better tomorrow ( BBT ) Unenepeshaji wa Ng'ombe .

3: Kituo cha Utafiti Mifugo ,  Mbegu bora za Marisho na Uzalishaji wa mbuzi wa kisasa na kondoo. ( TARIRI ) .

Shamba hilo ni moja ya mashamba makubwa ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Pongezi kwako Mbunge Mnyeti kwa kuumaliza mgogoro huo uliodumu muda mrefu hakika wewe ni kiongozi wa kuigwa. Kazi Iendelee. 

No comments

Powered by Blogger.