Header Ads

KAMPUNI YA AGRICOM AFRICA LIMITED YATAMBULISHA TREKTA MPYA KWA AJILI YA KILIMO CHA MPUNGA

Mkuu wa Uendeshaji wa Kampuni ya Agricom Afrika Limited, Elias Leasa, akiwaonesha zana za kilimo na matrekta ya aina mbalimbali waandishi wa habari (hawapo pichani) ilimo baada ya kufanya nao mahojiano maalumu ofisini kwake jijini Dar es Salaam Machi 14, 2025.

......................................

Na Dotto Mwaibale, Dar es Salaam

KAMPUNI ya zana za kilimo ya Agricom Africa Limited yenye makao yake makuu jijini Dar es Salaam imetambulisha trekta mpya aina ya Kubota L45 yenye uwezo wa 50 HP ambayo ina 4WD kutoka nchini Japan mahsusi kwa ajili ya kilimo cha  Mpunga.

Akizungumza katika mahojiano maalumu na  waandishi wa habari  Machi 14,2025 Ofisini kwake jijini Dar es Salaam,  Mkuu wa Uendeshaji wa kampuni hiyo, Elias Leasa, alisema kampuni hiyo ni ya kwanza hapa nchini kwa usambazaji wa zana bora za kilimo.

Alitaja matrekta mengine wanayo sambaza kwa wakulima nchini kupitia kanda walizoweka kuwa ni Kubota EK 4, Swaraj 975 na Swaraj 744 FE ambayo ni imara na yenye uwezo mkubwa wa kufanya kazi maeneo mengi na bei yake nafuu. 

No comments

Powered by Blogger.