KAMPUNI ZA CHAI KUTOKA JAPAN ZAWASILI NCHINI KWA ZIARA YA SIKU NNE
Kaimu Mkurugezi wa Bodi ya Chai Tanzania(TBT) Bi. Beatrice Banzi (wa pili kulia), akizungumza na wajumbe kutoka kampuni mbili za kutoka nchini Japan ambao wamekuja nchini kwa ziara ya siku nne.
.....................................
Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam
KAMPUNI mbili za chai kutokea nchini Japan, Nasa Corporation
na ITO EN Ltd zimewasili hapa nchini kwa ziara ya siku nne, zimepokelewa na
Kaimu Mkurugezi wa Bodi ya Chai Tanzania(TBT) Bi. Beatrice Banzi.
Viongozi wa kampuni hizo
wakiwa hapa nchini watatembelea mashamba ya chai na viwanda vya kuchakata
chai kwenye mikoa inayolima chai huku pia
wakifanya mazungumzo na wadau mbalimbali wa zao la chai ikiwemo, sekta
yaumma na binafsi.
Katika kuhakikisha ujio wao na uwekezaji wao unakuwa wenye
tija, TBT imeungana na wadau wa Taasisi Binafsi na Umma kama vile Kituo cha
Uwekezaji Tanzania (TIC) huku kwa upande wa sekta binafsi ipo kampuni ya Afri
Tea, African Pride, Kilimanjaro Teas na pia ipo
Taasisi isiyo ya Kiserikali ya Care International.
Ujio wa kampuni hizo mbili kubwa ni matokeo ya jitihada
zinazofanywa na Serikali ya Awamu ya
Sita chini ya uongozi wa Mheshimiwa Rais, Dk. Samia Suluhu Hassan kupitia
Wizara ya Kilimo na (TBT)ikiwa na lengo la kuliongezea thamani zao la chai
nchini kwa kuwavutia wawekezaji mbalimbali hususan kutoka nje ya nchi.
Kaimu Mkurugezi wa Bodi ya Chai Tanzania(TBT) Bi. Beatrice Banzi. akipokea zawadi utka kwa wajumbe wa kapuni hizo.
Mazungumzo na wajumbe hao yakifanyika
Zawadi ziipokelewa.






No comments