Header Ads

UCHUMI JUMUISHI WAPEWA MSUKUMO: ECONOMIC SOCIAL RESEARCH FOUNDATION NA FANRPAN WAKUTANA DODOMA KUJADILI MRADI WA MNYORORO WA THAMANI

 
Mkurugenzi wa Idara ya Maendeleo ya Mazao kutoka Wizara ya Kilimo, Dkt. Yasinta Nzogela, akizugumza wakati akifungua kikao cha Taasisi ya Economic and Social Research Foundation (ESRF), na FANRPAN ambazo zilikutana Machi 27, 2026 Jijini Dodoma kujadili mradi wa uchumi jumuishi.
..................................

Na Dotto Mwaibale, Dodoma

TAASISI ya Economic and Social Research Foundation (ESRF), inayojihusisha na tafiti za kisera na kutoa mapendekezo kwa taasisi za serikali na binafsi katika utekelezaji wa sera za nchi, kwa kushirikiana na FANRPAN, zimekutana jijini Dodoma kujadili mradi wa uchumi jumuishi.

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa kikao hicho, Mkurugenzi wa Idara ya Maendeleo ya Mazao kutoka Wizara ya Kilimo, Dkt. Yasinta Nzogela, ambaye alikuwa mgeni rasmi  alisema uchumi jumuishi ni mradi unaoratibiwa na FANRPAN, taasisi ya kikanda barani Afrika inayojihusisha na utafiti wa sera, huku ESRF ikiwa mratibu wa utekelezaji nchini Tanzania.

Alisema lengo kuu la mradi huo ni kuangalia namna ya kuwa na uchumi wa mzunguko ambapo hakuna rasilimali itakayopotea katika mnyororo wa thamani kuanzia uzalishaji shambani hadi kufika kwa mlaji.

“Maana yake ni kwamba kila kitu kiongezwe thamani na kutumika. Kwa mfano, mmea hutumia virutubisho kutoka kwenye udongo na kuzalisha chakula; binadamu na wanyama tunakula, kisha mabaki yanarejeshwa tena shambani kama mbolea, na mzunguko unaendelea,” alisema Dkt. Nzogela.

Alifafanua kuwa mzunguko huo unaohusisha matumizi ya maji, mbolea na uongezaji thamani mdogo mdogo ndiyo unaoitwa uchumi jumuishi, ambao pia umepewa kipaumbele katika dira ya maendeleo ya mwaka 2050, inayosisitiza utunzaji wa mazingira na uchumi endelevu.

Aidha, alisema kuwa kufikia uchumi wa kati kunahitaji kuimarisha dhana ya uchumi jumuishi, kwani inafungua fursa nyingi za ajira katika mnyororo wa thamani.

“Tukiangalia uchafu unaotokana na uzalishaji shambani, siyo uchafu bali rasilimali. Tukitumia teknolojia kuuchakata, tunaweza kupata mbolea ya asili (organic) yenye thamani kubwa kwa uzalishaji,” aliongeza.

Dkt. Nzogela alisisitiza kuwa utekelezaji wa dhana hiyo kuanzia uzalishaji hadi matumizi utasaidia kuinua uchumi wa wananchi na kulinda mazingira.

Kwa upande wake  Vivian Kazi ambaye ni Mtafiti Mkuu na Mkuu wa Kitengo cha Utafiti wa Kimkakati na Machapisho wa Taasisi katika Nyanja za Jamii na Uchumi ESRF alisema mradi huo wameuanza miaka mitatu iliyopita unaohusiana na uchumi jumuishi kwenye mfumo wa chakula.

Alisema mradi huo wameufanya kwa kushirikiana na Tanzania, Msumbiji pamoja na Zimbabwe na kuweza kuufanya katika kila nchi kuona namna gani sera zao zinajikita au hazijikiti katika kusaidia kupunguza uharibifu au upotevu wa mazao katika mchakato mzima tokea mazao yanapopandwa, kuvunwa mpaka mlaji wa mwisho.

Pia aliongeza kuwa ni jinsi gani wanaweza kupunguza upotevu huo kwa kutumia tena mabaki yote yanayotokana na chaakula kuanzia kinapozalishwa hadi kinapofika mezani na kinaporudishwa tena kuzalishwa kwa mara ya pili kwa maana kwamba mabaki yale kutumika kama mbolea lakini pia vyakula vya wanyama na kadharika.

“Tumefanya utafiti huu karibu na Chuo Kikuu Ardhi tukijikita zaidi upande wa sera ambazo zitaweza kushawishi watu wote wasiweze kutumia chakula vibaya ama mabaki yanayotokana na chakula ili kuweza kuyatumia tena na tena,” alisema Kazi.

Kuhusu, FANRPAN inaendelea kusaidia Tanzania kupitia midahalo ya sera za kilimo na chakula, ikilenga ushirikishwaji wa jamii, kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi na kuimarisha mifumo endelevu ya chakula kwa kushirikiana na taasisi za ndani kama ESRF.Bi. Vivian Kazi, Mtafiti Mkuu na Mkuu wa Kitengo cha Utafiti wa Kimkakati na Machapisho wa Taasisi katika Nyanja za Jamii na Uchumi ESRF, akizungumza kwenye kikao hicho. 

Kikao kikifunguliwa. Kutoka kushoto ni Mkurugenzi wa Idara ya Maendeleo ya Mazao kutoka Wizara ya Kilimo, Dkt. Yasinta Nzogela, Bi. Vivian Kazi, Mtafiti Mkuu na Mkuu wa Kitengo cha Utafiti wa Kimkakati na Machapisho wa Taasisi katika Nyanja za Jamii na Uchumi ESRF na Profesa Makarius Mdemu kutoka Chuo Kikuu cha Ardhi.

Mchumi Mwandamizi, Doris Sandewa akijitambulisha katika kikao hicho.

Profesa Makarius Mdemu kutoka Chuo Kikuu cha Ardhi. akichangia jambo kwenye kikao hicho.

Kikao kikiendelea

Afisa Mawasiliano wa ESRF Lilian Mfugale akichangia jambo kwenye kikao hicho.
Afisa Kilimo Mkuu Wizara ya Kilimo, Lilian Paschal akijitambulisha kwenye kikao hicho.

 Mkurugenzi wa Idara ya Maendeleo ya Mazao kutoka Wizara ya Kilimo, Dkt. Yasinta Nzogela (kushoto), na Bi. Vivian Kazi, Mtafiti Mkuu na Mkuu wa Kitengo cha Utafiti wa Kimkakati na Machapisho wa Taasisi katika Nyanja za Jamii na Uchumi ESRFwakiteta jambo kwenye kikao hicho.

Taarifa hii imeandaliwa na Dotto Mwaibale namba ya simu 0754362990

No comments

Powered by Blogger.