Header Ads

WANAFUNZI ST. ROSALIA SCHOOL NURSERY AND SECONDARY WAPATA UJI WA LISHE BANDA LA KAMPUNI YA LONG LIFE GROUP CO. LTD SABASABA



Wanafunzi wa St. Rosalia School Nursery Primary and Secondary ya Kinyerezi Tabata Mtaa wa Mkuyuni- Zimbili wakiwa  wamejipanga foleni kwa ajili ya kupata  Uji wa Lishe walipotembelea Banda la Kampuni ya Longlife Group Co.Ltd kwenye Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara Dar es Salaam Sabasaba Julai 10, 2026.

...........................

WANAFUNZI wa St. Rosalia School Nursery Primary and Secondary ya Kinyerezi Tabata Mtaa wa Mkuyuni- Zimbili Jijini Dar es Salaam wamepata Uji wa Lishe baada ya kutembelea Banda la Kampuni ya Longlife Group Co.Ltd kwenye Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara Dar es Salaam Sabasaba Julai 10, 2026.

Uji huo umepikwa kwa Unga wa Lishe unaotengenezwa na kampuni hiyo.

Kutokana na ubora wa uji huo umekuwa kivutio katika Maonesho hayo ambapo mamia ya watu wamekuwa wakifika katika banda la kampuni hiyo kuununua sanjari na Unga wa Lishe.

Unga huo ambao unaitwa Afya Meal ni mzuri kwa afya unatumiwa na watoto kuanzia miezi sita na watu wazima una mchanganyiko wa mahindi lishe, mbegu za maboga, mbegu za mchicha, maziwa soya na mbegu za chia.

Kampuni hiyo ndiyo mzalishaji na msambazaji mkuu wa bidhaa za chakula nchini Tanzania.

Aidha, kampuni hiyo inajulikana kwa kutengeneza unga wa lishe wenye chapa ya LF Lishe (Long Life Natural Foods), unaolenga kujenga afya ya familia na jamii.

Aina za Unga wa Lishe kutoka Long Life Group LF Nutritious Porridge (Unga wa Uji wa Lishe).

Unga huo ni mahususi kwa ajili ya kupika uji uliosheheni virutubisho na umelainishwa vizuri ili uwe rahisi kuyeyuka tumboni, ukitoa nguvu na kusaidia ukuaji bora wa watoto pamoja na watu wazima.

Unga mwingine unaotengenezwa na kampuni hiyo ni LF Dona Lishe (Unga wa Ugali wa Lishe)

Huo ni unga wa ugali ulio na virutubisho vya  asili (bio-fortified) kwa ajili ya kulinda na kuimarisha afya za familia kupitia mlo mkuu wa ugali.

Katika Maonesho ya Sabasaba yanayoendelea jijini Dar es Salaam mamia ya watu  wamekuwa wakifurika katika banda la kampuni hiyo kwa ajili ya kununua unga huo uliowekwa kwenye vifungashio vya kilo moja, nusu kilo na robo kilo na kuuzwa kwa bei nafuu.

Mbali ya uuzwaji wa unga huo pia wananchi wanaotembelea banda la kampuni hiyo  wamekuwa wakinunua uji uliopikwa na kuuzwa katika Maonesho hayo.

Wanafunzi wa shule hiyo wameishukuru kampuni hiyo kwa kuwa vinara wa uzalishaji wa Unga wa Lishe  ambao unajenga afya za jamii katika Taifa.

Wanafunzi wa St. Rosalia School Nursery Primary and Secondary ya Kinyerezi Tabata Mtaa wa Mkuyuni-Zimbili Jijini Dar es Salaam wakinywa Uji wa Lishe baada ya kutembelea banda la kampuni hiyo.

Wanafunzi wa St. Rosalia School Nursery Primary and Secondary ya Kinyerezi Tabata Mtaa wa Mkuyuni-Zimbili Jijini Dar es Salaam wakigongesha vikombe kufurahia kunywa Uji wa Lishe baada ya kutembelea banda la kampuni hiyo.

Habari hii imeandaliwa na Dotto Mwaibale simu namba 0754362990.

 

No comments

Powered by Blogger.