DKT. BITEKO AZINDUA TOVUTI RASMI YA NANENANE
Wizara ya Kilimo inawakaribisha Wakulima, Wafugaji, Wavuvi, Wafanyabiashara, Wawekezaji, Wazalishaji, Taasisi za Fedha na Wadau wote wa ndani na nje ya nchi kwenye mnyororo wa thamani katika Sekta ya Kilimo kushiriki maonesho hayo ambayo yanatoa fursa za kibiashara na za kujifunza teknolojia mbalimbali.
Kauli mbiu ya Nanenane Mwaka 2024 ni “Chagua Viongozi Bora wa Serikali za Mitaa kwa Maendeleo Endelevu ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi”.
Ili kupata nafasi ya banda la Maonesho tafadhali tembelea https://nanenane.kilimo.go.tz au piga simu namba 0712 310648 au Namba 0658 860870.


No comments