Header Ads

KIJUE KILIMO BORA CHA MIWA

Shamba la miwa.


Kilimo cha miwa ni kilimo chenye tija kwa mkulima, kilimo hiki kinaweza kufanywa na mtu yeyote yule aidha awe ameajiliwa au laaa.

Kuna aina kuu 2 za miwa:

1. BUNGALA

2. MIWA MYEKUNDU

Unachotakiwa kufanya katika kulima kilimo hiki ni, Kwanza kabisa tafuta aridhi.

Tafuta mbegu ya miwa ya BUNGALA miwa hii ni laini sana na ni rahisi kuichana kwa kutumia meno, baada ya kupata miwa hii kata vipande vipande vya pingili tatu.

Kumbuka kwamba miwa ni rahisi sana kushambuliwa na mchwa, Ili kuzuia isiliwe na mchwa nenda katika maduka ya kilimo na ununue viuatilifu au wasiliana nasi @kilimo_tz

FURSA

Soko la muwa ni kubwa sana, maana viwanda vingi vya sukari hapa Tanzania vinahitaji miwa, na mashamba ya miwa yaliopo hayatoshelezi mahitaji.

Hivyo viwanda hivi vya sukari viko tayari kununua miwa kutoka kwa wakulima ili kupata mahitaji ya maligafi ambayo ni miwa.

UPANDAJI WA MIWA

Hakikisha unapokuwa unapande miwa yako acha nafasi ya mita moja (1m) kati ya mche na mche, pia mita moja (1m) kati ya mstari na mstari.

Unapokuwa unapanda miwa hii hakikisha hizo pingili zote 3 zimezama ndani ya ardhi na kipande kidogo tu ndio kibakie juu ya uso wa ardhi, katika wa nyuzi 30.

Kwenye ploti ndogo ya mita 50 kwa mita 70, utakuwa na miche 70×50=3500 (mashina elfu tatu na mia tano).

SHARE NA NDUGU ZETU WENGINE ILI TULEGEZE VYUMA

INUKA Tanzania INUKA Afrika Mashariki- Ufugaji na Kilimo cha Kisasa

INAENDELEA.....

#kilimochamiwa #miwa #kilimochamiwa #mashambayamiwa #sokolamiwa #sukari #viwandavyasukari #sugarcane #sugarcanefarming #mbeguzamiwa #dripirrigationsystem #kilimochamatone #kilimochaumwagiliaji #kilimochakisasa

Simu:

+255 712 25 31 02(WhatsApp)

+255 692 43 02 63

Email:

kilimotz3@gmail.com

 

No comments

Powered by Blogger.