Header Ads

TARI KUSHIRIKIANA NA WAKULIMA KWENYE UTAFITI WA MBEGU

Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Kilimo Tanzania (TARI)

................................ 

Na Grace Hamisi, Mtwara

TAASISI ya Utafiti wa Kilimo Tanzania (TARI) inatarajia kuanza kushirikiana na wakulima kufanya utafiti wa mbegu bora.

Hayo yalisemwa na Mkurugenzi Mkuu wa TARI, Dkt. Thomas Bwana wakati wa ziara yake ya kikazi aliyoifanyi hivi karibuni  katika kituo cha utafiti wa kilimo (TARI) Naliendele ambapo pia alipata fursa ya kutembelea sehemu za uzalishaji wa miche ya mikorosho na michikichi pamoja na kiwanda cha kubangua korosho kilichopo kituoni hapo.

Dkt. Bwana alisema kuwa kwa sasa TARI imejipanga kuwashirikisha wakulima katika utafiti wa uzalishaji wa mbegu ili kusaidia na wao  kujitengenezea mbegu zilizo bora.

"Katika siku zijazo tunataka mkulima wa korosho awe na misimu miwili wa korosho, karanga na msimu wa bibo kwani siku hizi bibo linaonekana ni kitu cha kutupwa kumbe kuna bidhaa ambazo zinapatikana kama mvinyo (wine), Ethanol inayotokana na bibo pamoja na juisi ya bibo hivyo tunahakikisha kuwa tunapata bidhaa zote katika ngazi ya kibiashara," alisema Bwana.

Aidha Dkt Thomas meongeza kuwa (TARI) Naliendele imefanya vizuri kwenye utafiti wa korosho kwa upande wa magonjwa ya ubwiri unga huku aina nane (8) za mbegu za  korosho zilizofanyiwa utafiti na kubainika kuwa na uhimilivu mkubwa wa magonjwa.

Hata hivyo Dkt Bwana alisema kwa sasa wanataka kuwapa wakulima fursa ya kujaribu mazao tofauti na waliyoyazoea kama migomba na michikichi kutokana na mimea hiyo kuwa na uhitaji mkubwa  katika uazalishaji wa mafuta ambayo ni sehemu ya  mkakati wa kitaifa katika uzalishaji wa mafuta ili kuachana na uagizaji kutoka nje ya nchi.

No comments

Powered by Blogger.