TFC YASAMBAZA MBOLEA TANI 100,000 MSIMU WA KILIMO WA 2024/ 2025
Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya Mbolea Tanzania (TFC), Bw. Samuel Mshote akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake katika mahojiano maalumu yaliyofanyika Machi 13, 2025 jijini Dar es Salaam.
................................
Dotto
Mwaibale na Angelina Mganga
KAMPUNI ya
Mbolea Tanzania (TFC) katika kipindi cha msimu wa kilimo cha 2024/2025 imeweza kusambaza tani 100,000 za mbolea aina
tofauti tofauti.
Hayo yamebainishwa
na Mkurugenzi Mkuu wa kampuni hiyo, Samuel Mshote wakati akizungumza na waandishi
wa habari ofisini kwake katika mahojiano maalumu yaliyofanyika Machi 13, 2025.
Alisema mbolea iliyosambazwa tani 30,000 ilikuwa kwa ajili ya kupandia, tani 25,000 ya kukuzia na kuwa wanaendelea kuipokea kutoka nje ya nchi pamoja na tani 15,000 aina ya UREA kwa ajili ya kunenepesha mazao.
Mshote alisema TFC ni Taasisi ya Serikali inayojitegemea ambayo ilianzishwa mwaka 1968 chini ya Sheria ya Makampuni (Companies Ordinance CAP 212)
Alisema kampuni hiyo inatimiza malengo yake kwa kufanya kazi kwa misingi ya kibiashara na kuwa inafanya uwekeza ili iweze kupata faida na kuwa kazi yake kubwa ni kuzalisha mbolea na viatilifu.
Alisema
malengo makuu ya kampuni hiyo ni kuzalisha mbolea, kuagiza kutoka nje ya nchi
na kuwauzia wakulima wa ndani ili wapate mbolea iliyo bora na yenye kukidhi mahitaji.
Alitaja malengo mengine ya kampuni hiyo ni kuhakikisha bidhaa hiyo inapatikana katika kipindi chote cha mwaka na kwa bei nafuu.
“ Malengo mengine ni ya kimkakati ya
kuhakikisha tunaingiza na kufunga kiwanda kwa ajili ya kuchanganya
mbolea ambazo zitaendana na afya ya udongo ya maeneo tofauti tofauti ya nchi
yetu ili kuweza kuwahudumia wakulima kuwapatia mbolea zinazoendana na afya ya
udongo katika maeneo wanayolima ili kuongeza tija,” alisema Mshote.
Aidha,
Mshote alisema wanaendelea kufanya tafiti mbalimbali zinazoweza kuleta
maendeleo kupitia pembejeo, mbolea pamoja na madawa yake.
Mshote
aliongeza kueleza kuwa kampuni hiyo pia inatoa huduma za pembejeo za mbolea kwa
ajili ya zao la Tumbaku ambapo jumla ya tani 61,000 ya mbolea aina ya NPK
101824 zilipelekwa, tani 10,700 za CAN pamoja na UREA tani 2021.
Alisema kwa kipindi chote cha usambazaji wa mbolea
wameweza kusamba jumla ya tani 73,000 na kwenye mazao ya kawaida wamepeleka tani
75,000 na kueleza kuwa kwa kampuni hiyo ni
historia kwani hawajawahi kusambaza mbolea kwa kiasi hicho kwa wakulima wa
kawaida na wa zao hilo la Tumbaku.
Mkurugenzi
Mshote alitumia nafasi hiyo kumshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Samia
Suluhu Hassan kwa kuweza kuifufua kampuni hiyo na kusaidia kupata uongozi kwa
maama bodi ya ya Wakurugenzi, Menejimenti pamoja na kuiamini na kuwapatia mtaji
wa fedha ili iweze kujiendesha kibiashara.
Alisema fedha hizo zimetolewa ili wakulima wapate mbolea na kufanya kilimo chenye tija na kuleta usalama wa chakula nchini lakini pia kutimiza malengo makubwa ya Serikali ya kilimo kichangie pato la Taifa kwa asilimia 10 ifikapo mwaka 20/30.
Aidha, Mshote amemshukuru Waziri wa Kilimo Mhe. Hussein Bashe kwa kuwa nao bega kwa bega na kutoa
miongozo mbalimbali, ushauri na maelekezo ya namna gani yakufanya kazi kwa
ubunifu na kuweza kuwafikia wakulima wengi na kupata mbolea na viatilifu na
kuvisambaza kote nchini kwa weledi na ubora wa hali ya juu.
“ Tuna
muhakikishia waziri wetu kuwa TFC inafanya vizuri kazi na inalinda fedha za umma
na inapata faida na kuweza kujiendesha kibiashara,” alisema Mshote.
Akielezea
hali ya usambazaji wa mbolea alisema kampuni inaisambaza nchi nzima kupitia
maghala , vituo vya mauzo na kuwa kuna maeneo wana maghala yenye uwezo wa kuhifadhi mbolea hadi tani 100,000.
Alisema maghala
hayo Mkoa wa Mwanza (Mjini) ,Mbeya (Mbalizi), Sumbawanga, Njombe, Makambako, Ruvuma,
Songea na Tunduma.
Pia alisema kuwa wana jumla ya mawakala
600,000 ambao wanatumika kusambaza mbolea za Ruzuku za Serikali pamoja na kusajili vyama 29 vya ushirika kwa ajili ya kusambaza
mbolea kwa wakulima.
Alisema mahitaji
makubwa ya mbolea yapo katika mikoa ya
Nyanda za Juu Kusini ambayo ni Mbeya, Songwe, Makambako, Iringa, Morogoro, Songea
na Sumbawanga.
Alisema
matumizi ya mbolea kwenye kilimo yameongezeka kutoka tani 360,000 hadi kufikia
tani 800,000 kwa mbolea zinazosambazwa
kwa ruzuku za serikali.
Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya Mbolea Tanzania (TFC), Samwel Mshote akisisitiza jambo kwenye mkutano huo na waandishi wa habari.
Wanahabari wakiwajibika wakati wa mahojiano hayo.



No comments