SOSEJI ZA DR. FLAVE: ZAWA GUMZO, ZAWALIZA WATOTO, ZINAPATIKANA MIKOCHENI B JIJINI DAR ES SALAAM
Muonekano wa Soseji za Dr. Flave
.............................................
Na Dotto Mwaibale, Dar es Salaam
SOSEJI ni chakula kilichotengenezwa
kwa nyama iliyosagwa au kukatwa kwa vipande vidogo, kuchanganywa
na chumvi na viungo halafu kujazwa katika sehemu
za utumbo au mirija ya plastiki. Kwa aina mbalimbali
za soseji viwango vya nafaka au mkate vinaweza kuongezwa
katika mchanganyiko.
Jina soseji
limeingia
katika Kiswahili kutoka Kiingereza "sausage"; asili yake
ni Kilatini "salsica" yenye maana ya "iliyotolewa
chumvi".
Vipande
virefu vinavyotokea baada ya kujaza hutenganishwa kwa kufunga sehemu kwa kamba au
kuviringisha vipande vinavyoweza kukatwa baada ya kupika.
Soseji
nyingi hupikwa baada ya kutengenezwa. Aina nyingine zinawekwa katika moshi juu
ya moto zikiiva humo
kwa muda wa siku au wiki kadhaa. Aina kadhaa
hukauka tu hewani.
Soseji za kupikwa zinaweza kufungwa katika makopo maalumu au glasi ambako zinaweza kudumu kwa muda mrefu.
Halikadharika huwekwa kwenye mifuko au vifungashio maalumu na hutunzwa kwa kuwekwa kwenye majokofu (Friji) kwa zile ambazo ni fresh ila zingine huhifadhiwa kwenye vifungashio hivyo malumu na kutunzwa kwenye mazingira ya baridi la kawaida.
Siku
hizi soseji hutengenezwa mara nyingi kiwandani kwa kutumia mashine zinazosaga
nyama nyingi na kutengeneza soseji mfululizo.
Soseji
zimetengenezwa tangu kale. Kwa upande moja ni njia ya kutunza nyama kwa muda
kabla ya matumizi kwa kuongeza chumvi inayoozuia bakteria na kuziweka
katika moshi inayozuia wadudu kutaga mayai kwenye soseji.
Mbinu hiyo ni vigumu katika mazingira ya joto pasipo jokofu.
Soseji
zinaweza kuliwa peke yake, pamoja na mkate baridi, zinaweza kupikwa
pamoja na mboga ya majani..
Ziko
aina zinazofaa kuliwa bila kupashwa moto.
Nchi
nyingi na hata mikoa kadhaa huwa na soseji za pekee zinazotofautiana
katika ladha na mwonekano.
Lengo
la kuanza na utangulizi huu ni kutaka kueleza kwa kifupi jinsi ya kitoweo hicho kinavyo tengenezwa na
leo napenda kuzungumzia Soseji za Dr. Flave zinazotengenezwa na Kampuni ya Dr. Flave kwa kushirikiana na Kilimo Joint
yenye ofisi zake Mikocheni B Jijini Dar
es Salaam.
Soseji
za Dr. Fave zimejizolea umaarufu mkubwa na kutokewa kupendwa na wakazi wa Dar
es Salaam na maeneo mengine ya nchi kutokana na kuwa na ladha nzuri na kuzifanya soko
lake kuwa kubwa.
Hali
hiyo inatokana na jinsi zinavyotengenezwa na kuandaliwa na wataalamu wa mapishi
ambao ni wabobezi wa kimataifa na kuzifanya zinunuliwe na watu kutoka ndani ya
nchi na mataifa mbalimbali na bei zake ni nafuu.
Meneja
Masoko wa kampuni hiyo Linda Byaba anasema
kampuni yao inajishughulisha na ufugaji wa kuku, kuku wa nyama na kuku
wa mayai na pia kutoa ushauri wa ufugaji pamoja na uzalishaji wa soseji za
ng’ombe maarufu kama soseji / mtura.
“Soseji zetu zimetokea kupendwa hasa na watoto
ambao wazazi wao wamekuwa wakipongeza kutokana na kutengenezwa kwa viwango vya
juu na kuwa na ladha nzuri ambao mara kwa mara wamekuwa wakitoa oda kwa ajili
ya watoto wao ambao wamekuwa wakizililia kutokana na utamu wake,” alisema Byaba.
Alisema
kampuni hiyo inaziandaa soseji hizo ambapo wateja wao wanakwenda kuzipika
kulingana na mahitaji ya mapishi yao binafsi majumbani kwao na mahotelini.
Akizungumzia
upatikanaji wa soseji hizo, Byaba alisema wanapokea oda kutoka mikoa mbalimbali
hapa nchini ikiwemo Mwanza, Iringa,
Mbeya na kuwa bidhaa hiyo inawafikia kwa wakati mara baada ya kukamilisha
malipo.
Meneja masoko huyo anasema wanamzigo wa kutosha wa Soseji za Dr.
Flave na kuwa sasa zinapatikana kuanzia
nusu kilo na kilo na kuwa oda za mikoani wanazipokea siku mbili kabla.
Alisema mteja au mtu yeyote anayehitaji soseji hizo anaweza kuwasiliana na Dr. Flave na kutoa oda kupitia Instagram yao @dr.flave2 au @dr.flave au WhatsApp au kwa namba ya simu ya
kawaida ambayo ni 0677303000
Soseji za Dr. Flave
No comments