WAADHIRI CHUO CHA MIPANGO NA WANAFUNZI KUTOKA CHINA WAKUTANA DODOMA KUJADILI KILIMO CHA NGANO
Waadhiri wa Chuo cha Mipango jijini Dodoma wakiwa katika picha ya pamoja baada ya kufanya mdahalo uliohusu kilimo bora cha zao la ngano.
...................................
Na Mwandishi Wetu, Dodoma
WAADHIRI wa Chuo cha Mipango jijini Dodoma wakishirikiana na Wanafunzi wa kutoka nchini China wamefanya mdahalo wa namna bora ya kufanikisha cha kilimo cha kisasa katika zao la ngano ambalo awali limekuwa likiagizwa nje ya nchini.
Wakizungumza jijini Dodoma baadhi ya waadhiri kutoka chuo hicho wamesema wameona wafanye ushirika na wanafunzi kutoka nchini china ili kubadilishana mawazo na mbinu, wakijikita zaidi katika kilimo cha ngano ambacho bado nchi inahitaji kufikia mafanikio zaidi katika kuendesha kilimo hicho.
Mmoja wa Wanafunzi kutoka nchini China ametoa maoni juu ya kufikia mafanikio hayo akieleza moja ya hatua inayotakiwa kuchukuliwa kwa haraka ni kuboresha miundo mbinu ili iwe rahisi kwa mkulima kutoka sehemu moja kwenda sehemu nyingine.
Mdahalo ukiendelea
Mdahalo ukiendeleaMaelezo ya mkakati huo yakichukuliwaWanafunzi kutoka nchini China wakiwa kwenye Mdahalo huo.









No comments