UZALISHAJI WA MAWESE KUONGEZEKA NCHINI
Msukumo mpya wa uzalishaji utaelekezwa katika mkoa wa Kigoma, ukanda wa
kilimo cha jadi cha michikichi na baadaye mikoa mingine ikiwamo Mbeya.
Taasisi ya Utafiti wa Kilimo Tanzania (Tari) kupitia vituo vyake vya Tumbi na Kihinga katika mikoa ya Tabora na Kigoma watajumuishwa katika mpango wa mafuta ya mawese.
Chanzo:- Dr.Dwi Asmono, Mkurugenzi wa Kampuni ya Biashara ya Kilimo ya
Indonesia iitwayo Sampoerna Agro
Mkoa wa Kigoma unazalisha 80% ya mafuta ya mawese kila mwaka.
Makampuni ya Indonesia yataungana na Tari na taasisi washirika katika
kuanzisha aina za michikichi zinazozaa kwa wingi kupitia utumiaji wa mbinu
sahihi za kilimo.
Hivi sasa, inakadiriwa kuwa 80% ya mafuta ya kupikia yanayotumiwa nchini
Tanzania yanatokana na mafuta ya alizeti, hivyo ongezeko la mafuta ya mawese
itaifanya Tanzania kuwa na mafuta toshelevu kwa matumizi ya ndani na kuuza nje
ya nchi.



No comments